Pages

BRAND NEW MUSIC

metty magese

metty magese

Listen & Download

http://mdundo.com/a/32626

Tuesday, January 31, 2012

MTUME NA NABII MWINGIRA ATIWA MBARONI DAR

KIONGOZI wa Kanisa la Efatha, Nabii na Mtume Josephat Mwingira amekamatwa na polisi  katika Kituo cha Polisi cha Oysterbay, Dar es Salaam, akituhumiwa kuharibu mali za mfanyabiashara, Zain Sharifu.

Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kipolisi, Kinondoni, ACP Charles Kenyela, Mwingira alikamatwa wiki iliyopita na kushikiliwa kituoni hapo.
Hata hivyo, Kenyela alisema, Mwingira alidhamiwa baada ya kuhojiwa kuhusiana na tuhuma za kuvunja na kuharibu mali ndani ya Kiwanda cha Uchapaji cha Afroplus kinachomilikiwa na mlalamikaji.

“Tumemkamata kiongozi huyo ili atoe ufafanuzi wa kina baada ya kupokea malalamiko hayo, “ alisema Kenyela alipozungumza na mwandishi wetu wiki iliyopita ofisini kwake.
Kenyela alisema, mashtaka hayo yalifikishwa polisi na Zain, Januari 8, mwaka huu, akidai kwamba walinzi binafsi wa kiongozi huyo wa kanisa, walivamia kiwandani kwake na kuharibu mali baada ya kufanya fujo.

Aliongeza kuwa polisi baada ya kupata taarifa hizo, walikwenda eneo la tukio kushuhudia na kukuta mali zilizoharibiwa, hivyo walimtaka Mwingira kufika polisi ili atoe ufafanuzi lakini alikaidi ndipo polisi ikatumia nguvu kumkamata.

“Alipoulizwa Mwingira kuhusu madai hayo alijitetea uwa eneo hilo ni mali halali ya Efatha tangu Juni 17, 2005, baada ya kulinunua kutoka kwa mtu mmoja aliyemtaja kwa jina la Mangula, hivyo anasubiri tamko la Mahakama ya Ardhi Tanzania ambako shitaka limepelekwa,” alisema.
Baada ya Mwingira kuhojiwa kituoni hapo, Kenyela aliwakutanisha na Zain ambaye ni mlalamikaji na kuwataka wasiendelee kugombana, badala yake wasubiri uamuzi wa mahakama kuhusu kesi hiyo.
Kamanda Kenyela alifafanua kuwa mwanamke aliyemshitaki Mwingira ni mmoja wa wamiliki 11 wa viwanda vilivyokuwa ndani ya Kitalu namba 90, Mwenge, Dar es Salaam.

Awali, Mwingira alisema, aliwataka wamiliki wa viwanda hivyo kuhama ili kupisha upanuzi wa kanisa na viwanda 10 vilitekeleza ombo hilo.
Uchunguzi wa gazeti hili umebaini kuwa makampuni 10 ambayo yalitakiwa kuhama na Mwingira na kutekeleza ni Metal Works, Timber Malt Tech, Auto Ran Makongo, Container Global, Simon Engineering, Safe Man, Profession Investigation, Elbe Ltd, Zana za Kilimo Mbeya na Kilimanjaro Machine Tools Ltd.

Januari 17 mwaka huu, katika toleo lake namba 721 gazeti hili liliripoti kusakwa kwa Mwingira na askari 20 waliofika kanisani kwake kwa lengo la kumkamata.
Askari hao waliokuwa katika magari mawili aina ya Land Rover ‘Difenda’ walifika kanisani kwa Mwingira baada ya kupata taarifa za kutokea kwa fujo kati ya wafuasi wa kanisa na wafanyakazi wa viwanda cha Afroplus kinachopakana na kanisa hilo, Mwenge, Dar lakini walimkosa.

Kamanda Kenyela alisema alimtuma mkuu wa polisi wa wilaya (OCD) kumpelekea Mwingira barua ya wito ili afike ofisini kwake na kutoa onyo kwamba kama akikaidi, wao polisi wasilaumiwe.
Baadhi ya wananchi waliokuwa katika Kituo cha Polisi cha Oysterbay baada ya kumuona Mwingira walisema ni kitendo cha aibu kwa viongozi wa makanisa ya kiroho kufikishwa polisi.

“Siyo Mwingira tu, tumekuwa tukiona viongozi wengi wa makanisa ya kiroho wakifikishana polisi na watu au wao kwa wao, ningeshauri haya mambo wayamalize kwa kuelewana uraiani. Wana uwezo wa kuombea matatizo, hilo linawashinda nini? Zamani ilikuwa ni mwiko kuona kiongozi wa dini akifika polisi kulalamika au kulalamikiwa,” alisema mama mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Frida Gabriel aliyedai kuwa ni mlokole.

MBUNGE VS DOKTA/MUUGUZI

Mhhhhh!!! Mi Simo,
Wamenitumia tu hawa wadau!

NAHODHA WA TWIGA STARZ KUKIPUTA UTURUKI

Nahodha wa timu ya Taifa ya mpira wa miguu ya wanawake (Twiga Stars), Sophia Mwasikili ameondoka jana alfajiri (Januari 30 mwaka huu) kwa ndege ya Turkish Airlines kwenda Uturuki kucheza mpira wa kulipwa.
 
Mwasikili amekwenda kujiunga na Luleburgazgucu Spor Kulubu inayoshiriki Ligi Daraja la Kwanza ya Wanawake nchini humo.
 
Beki huyo wa kati wa Twiga Stars aliyekuwa akichezea timu ya Sayari Women amejiunga na klabu yake hiyo mpya kwa mkataba wa miaka miwili.
 
Awali Mwasikili alitakiwa kujiunga mapema na timu hiyo lakini alilazimika kusubiri kwanza mechi ya marudiano ya Kombe la Afrika kwa Wanawake (AWC) kati ya Twiga Stars na Namibia (Brave Gladiators) iliyochezwa Januari 29 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam

WIZI WA KAZI ZA SANAA KISHA KAZI

Kaimu Katibu Mtendaji wa BASATA, Godfrey Lebejo akisisitiza jambo kwenye programu ya Jukwaa la Sanaa inayofanyika kila wiki makao makuu ya Baraza hilo Ilala Sharif Shamba na kuhudhuriwa na wadau wa Sanaa. Kulia kwake ni Afisa Uhusiano wa Uhamiaji Bi. Tatu Burhan.
Ssp Edson Kasekwa kutoka Jeshi la Polisi Makao Makuu, Kitengo maalum cha Operesheni uzuiaji uhalifu akitoa ufafanuzi wa masuala mbalimbali kuhusu matumizi ya Sanaa katika Polisi Jamii na Ulinzi Shirikishi. Kulia kwake ni Mkurugenzi wa Ukuzaji Sanaa, BASATA Bi. Vivian Shalua.
Afisa Uhusiano wa Idara ya Uhamiaji Tatu Burhan akieleza haja ya Jamii kushirkiana na Idara yake katika kupambana na tatizo la Uhamiaji haramu nchini. Kushoto kwake ni Bw. Lebejo.
Kikundi cha Ngoma cha Jeshi la Polisi kikitumbuiza kwenye Programu ya Jukwaa la Sanaa ambapo elimu kuhusu dhana ya Ulinzi Shirikishi na Polisi Jamii ilitolewa kwa Wadau zaidi ya 140.
Sehemu ya Maafisa wa Jeshi la Polisi wakifuatilia matukio mbalimbali kwenye Programu hiyo ya Jukwaa la Sanaa.
Mkongwe wa Sanaa za Maonyesho Mzee Nkwama Bhallanga akielezea masuala mbalimbali kuhusu Sanaa Shirikishi katika Polisi Jamii na Ulinzi Shirikishi.
Wadau wa Sanaa wakiifuatilia Programu ya Jukwaa la Sanaa wiki hii.

Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) na Jeshi la Polisi nchini wameunda kikosikazi maalum kitakachokuwa kikifuatilia uharamia na maovu mbalimbali katika shughuli za Sanaa na Burudani.

Kikosikazi hicho kimeundwa baada ya Jeshi la Polisi nchini kutumia Sanaa shirikishi katika kutoa elimu kwa wadau wa Sanaa kuhusu dhana ya polisi jamii na ulinzi shirikishi kwenye Jukwaa la Sanaa linalofanyika kila wiki makao makuu ya BASATA Ilala Sharif Shamba.

DJ CLEO WA FACEBOOK KUJA BONGO



Lebo ya OTHENTIC ambayo ndio inasimamia kazi za wasanii kadhaa wa bongofleva kama YOUNG DEE, imetangaza kumleta bongo kwa ajili ya show DJ CLEO, staa wa hit single ya FACEBOOK kutoka AFRIKA KUSINI.

C.E.O wa OTHENTIC producer Max amesema wako kwenye mazungumzo na wamefikia pazuri,  ambapo siku hiyo CLEO atasindikizwa na wakali wengine wa bongo kama Young Dee, Cosby, CP na wengine.

Amesema japo wameiandaa wao, pia wasanii wa lebo nyingine hapa bongo watapewa mwaliko wa kuperfom, japo list itakua ndogo.

show itafanyika march mwaka huu DAR ES SALAAM kwa ajili ya wanafunzi na wengine watakaopenda.

UZINDUZI WA LEBEL YA NE-YO JAMAICA

This past weekend Keri Hilson, Adrienne Bailon and Shaggy were spotted in Jamaica celebrating the launch of Ne-Yo’s new record label, Compound Island. Guests in attendance were treated to the Red Tails movie premiere, a performance at the annual Jazz Festival and a pool party at Secrets Resort.
In addition to starting his own label, Ne-Yo was recently appointed VP of A&R at Motown Records.  Meanwhile, Adrienne Bailon was released from Def Jam and signed a management deal with Ne-Yo’s Compound Entertainment.

RIHANNA NA DRAKE PAMOJA TENA UK

Oh na na! 
Drizzy Drake and his long time crush red hot Rihanna will be headlining a concert together in the UK. 
Drake and RiRi are all set to perform at this year's Wireless Festival in Hyde Park, London in July 2012. Drake is currently scheduled to hit the main stage on July 7th, while Rihanna is set to hit the stage a short 24 hours after her old Canadian boo.
Drizzy and RiRi aren't the only hot acts scheduled to hit the stage, Wiz Khalifa, Jessie J and Calvin Harris will also perform at this year's Wireless Festival. 

SHAGGY KUDONDOKA 12 FEB

shaggy-summer-in-kingston-dancehall-artiste.jpgInternationally acclaimed superstar, Shaggy will unleash a new version of his Grammy-nominated album, Summer in Kingston in February.
The eight-track digital album, originally released last July, will now be released in CD form, with two additional tracks. The release of the Summer in Kingston CD will take place around the time of the 54th annual Grammy Awards on February 12 in Los Angeles.
Shaggy explained the re-release during a recent interview with Splash; intimating that this version of Summer in Kingston will provide a different flavor.
"Initially we released the album digitally with eight songs and sold it at a fan appreciation price for a limited time. Now we are releasing the physical copy with a total of 10 songs, so it's now a full-length album," he said.
The new singles that will feature on the album include the Sly and Robbie produced, She Give Me Love as well as Hurting. Additionally, there'll be a new version of his new single, Dame, featuring Dominican-American singer, Kat DeLuna.

Monday, January 30, 2012

JOKATE AMPAKA WEMA KIJANJA

   MSANII aliyewahi kuwa Miss Tanzania namba mbili 2006, Jokate Mwegelo, amesema kuwa fani hiyo ya urembo imekuwa kama kimbilio la wanawake wahuni kitu ambacho kinachangia kuifanya ikose heshima yake kama ilivyokuwa zamani.

Mrembo huyo mwenye heshima katika fani hiyo, alisema kuwa endapo kutakuwa na sheria ambayo inambana miss yoyote ambaye anaokekana kwenda kinyume basi wanawake ambao wangependa kushiriki fani wangekuwa ni wale wenye tabia njema pekee.


Alisema kuwa wapo wengine ambao wanatabia nzuri lakini baada ya kushiriki katika fani hiyo wanabadilika na kufuata tabia za watu wahuni huku wakizani ni nzuri wakati ndiyo wanapoteza sifa zao kama warembo.


Alisema fani hiyo ni kazi kama nyingine hivyo kunapotokea mtu mwingine anaivunjia heshima anasababisha hata warembo wengine waliotamani kushiriki kukata tamaa kwa kuhisi endapo na yeye akishiriki anaweza kuwa na tabia za mtu fulani.


“Unajua hakuna kitu kibaya kama kuichafua kazi ambayo imekutoa kwa sababu kuna mtu mwingine anakuwa anatamani kushiriki fani hiyo, lakini kutokana na tabia aliyonayo mtu fulani ambayo si nzuri basi inakuwa inakatisha tamaa na wengine kushiriki,”
Alisema.

WATU 40 WAULIWA NA WEZI WA MIFUGO SUDAN


Wafugaji Sudan Kusini
Kambi za wafugaji Sudan Kusini
Maafisa wa serikali katika Sudan Kusini wanasema watu wasiopungua 40 wameuwawa na kundi la watu wenye silaha waliokwenda kuiba mifugo.
Baadhi ya taarifa zinasema idadi ya watu waliouwawa ni zaidi ya 100 kwenye uvamizi, huo uliotokea kwenye kambi moja katika jimbo la Warrap.
Waziri wa mambo ya ndani wa Sudan Kusini ameilaumu serikali ya Sudan kwa kuwapa silaha washambuliaji hao, ambao ni kundi la wapiganaji kutoka jimbo jirani la Unity.
Mvutano umeendelea kuwepo tangu Sudan Kusini ilipojitenga kutoka Sudan mwezi Julai, kufuatia vita vilivyochukua miaka mingi.
Afisa ammoja katika jimbo la Warrap ameambia gazeti la Sudan Tribune linaloandikiwa mjini Paris kwamba vijiji vinavyokaliwa na watu wa jamii ya Luac Jang katika wilaya ya Tong mashariki walishambuliwa Jumamosi alfajiri.
Spika wa bunge Madot Dut Deng amesema ameambiwa na maafisa kwamba zaidi ya watu 76 wameuwawa, na wengine hajulikani walipo.
Afisa mwingine katika jimbo hilo aliambia gazeti hilo watu katika eneo lililoshambuliwa wanasema waliouwawa ni zaidi ya 100.
Waziri wa mambo ya ndani Alison Manani Magaya amesema mashambulizi hayo yaliendeshwa na kundi la wapiganaji kutoka jimbo jirani la Unity.
"kundi hili lilipewa silaha na serikali ya Khartoum," aliambia gazeti la AFP, lakini hakutaja ni kundi gani.
Sudan Kusini ilipata Uhuru tarehe 9 Julai mwaka 2011 kufuatia vita vya wenyewe kwa wenyewe na Sudan.
Tatizo lililochangia mzozo hadi sasa ni kwamba silaha nyingi zimezagaa.
Silaha hizo zinatumika katika mapigano ya kikabila, ambayo mara nyingi yanahusu mifugo kutokana na umuhimu wake miongoni mwa jamii nyingi katika Sudan Kusini.
Katibu mkuu wa Umoja wa mataifa Ban Ki-Moon siku ya Jumapili alitoa wito kwa viongozi wa Sudan na Sudan Kusini kufanya makubaliano kuhusu namna ya kugawana utajiri unaotokana na mafuta, ambayo husababisha mvutano baina ya nchi hizo mbili.

DKT SHEIN AKUTANA NA AFISA WA UNDP IKULU DAR

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akisalimiana na Mwakilishi Mkaazi wa UNDP nchini Tanzania Dk. Alberic Kacou,alipofika Ikulu Mjini Zanzibar jana.Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akizungumza na Mwakilishi Mkaazi wa UNDP nchini Tanzania Dk. Alberic Kacou,alipofika Ikulu Mjini Zanzibar jana
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akizungumza na Mwakilishi Mkaazi wa UNDP nchini Tanzania Dk. Alberic Kacou,alipofika Ikulu Mjini Zanzibar jana.

JK HANDS OVER ALMA CHAIR TO PRESIDENT ELLEN JOHNSON SIRLEAF OF LIBERIA

A cross section of  African Leaders Malaria Alliance (ALMA)  leaders at the working session luncheon at the Africa Union Summit during which out-going Chairman President
Jakaya Mrisho Kikwete handed over the ALMA chair to President Ellen Johnson Sirleaf in the side-lines of the AU Summit in Addis Ababa, Ethiopia. ALMA is an alliance of African Heads of State and Government working to end malaria-related deaths. This body was founded by African Heads of State to utilize their individual and collective power across country and regional borders:
  New ALMA Chair President Ellen Johnson Sirleaf confers to out-going chair President Jakaya Mrisho Kikwete an award of Excellence from  the UN Secretary General and the African Union Chairman
for sound policies and effort to combating malaria
President Jakaya Kikwete makes his opening speech and give the status of Malaria. Others from left is the new AU Chairman President of Benin, the Executive Secretary of ALMA, Ms Joy Phumaphi , new ALMA Chair and President of Liberia Madame Ellen Johnson Sirleaf, and newly elected ALMA Vice Chair and President of Mozambique, Mr Armando Guebuza

RITA DOMINIC NDANI YA BIFU ZITO NA STEPANIE OKEREKE

MWIGIZAJI Stephanie anazidi kupata maadui baada ya Rita Dominic kuingia kwenye listi ya watu wanaompinga baada ya kupewa shavu nene katika tasnia ya filamu Nollywood.
Awali Stephanie aliyekua rafiki mkubwa wa Gienevieve Nnaji waliingia katika bifu baada ya Stephanie kupewa shavu hilo na yeye kupigwa chini.
Kisa cha kutokuwa na maelewani kwa wasanii hao ni kitendo cha Stephanie kuteuliwa kuwa kiunganishi kati ya wasanii na rais wa nchi hiyo, Goodluck Jonathan.
Gienevieve alipinga uteuzi huo akisema hawawezi kufanya kazi na rais halafu mtu wa katikati awe msanii huyo akidai kuwa bado mchanga.
Rita naye ameibuka na kusema kuwa anataka kuonana na rais lakini suala la eti kupitia kwa Okerekea analipinga kwa kuwa msanii huyo ni mdogo sana kwake.
"Stephanie ni nani hapa Nollywood, eti nikitaka kuwasiliana na rais lazima nimuone yeye, huyo aliyemteua ha


MAISHA WANAYOISHI WACHEZAJI WA AZAM FOOTBALL CLUB

Huyo ni mchezaji HIMID MAO, katika kila chumba wanakaa wawili wawili tu.
Kila chumba kina AC, choo na bafu,DSTV fulltime, kila mtu ana kitanda chake, kambi yao iko pembeni ya uwanja wao, Mbagala Chamazi.

UZEMBE WA DEREVA WASABABISHA VIFO VYA WATU WATANO

Kutoka eneo la tukio mmoja Kati ya abiria walionusurika katika ajali hiyo John Sanga alisema kuwa dereva wa basi hilo alikuwa akiendesha basi kwa mwendo kasi na uzembe mwingina hata abiria walipojaribu kumkanya alishindwa kusikiliza. Katika ajali hiyo abiria wengine zaidi ya 16 walijeruhiwa vibaya na kulazwa katika hospital ya wilaya ya Mufindi huku wengine zaidi ya 20 wakipata michubukomidogo midogo na kutibiwa na kuruhusiwa .Mashuhuda wa ajali hiyo walimweleza mwandishi wa habari hizi kuwa ajali hiyo ilitokea majira ya saa 9 alasiri Leo wakati basi hilo likielekea mkoani Mbeya na kuwa chanzo ni mwendo kasi na uzembe wa dereva. Alisema eneo hilo ambalo ajali imetokea ni eneo ambalo linamteremko na kuwa mbali ya basi hilo kupinduka pia magari mengine Mawili likiwemo gari la serikali lenye namba za usajili STK 2340 na IT yamegongana na Lori katika eneo hilo. Maiti zilizotolewa katika ajali hiyo hadi saa 2.usiku zilikuwa ni nne na hadi mwandishi wa habari hii anatoka eneo la tukio jitihada za kunyanyua basi hilo ilikutazama maiti nyingine lilikuwa likieendelea chini ya usimamazi wa mkuu wawilaya ya Mufindi Evarista Kalalu na mkuu askari wa Kikosi cha usalama barabarani wakiongozwa na mkuu wa kikosi cha usalama barabarani mkoa wa Iringa Kedmundi Mnubi lilikuwa likiendelea . Majeruhi wa ajali hiyo ambao wamelazwa katika hospital hiyo ya wilaya ya Mufindi ni pamoja na mtoto wa kiume wa mwaka mmoja ambaye mama yake alikufa katika ajali hiyo , Alen Kilima mkazi wa Kyela , Mwanahabari wa radio Kyela Fm Prakseda Mburu (24) ,Maria Mtawa (46) mkazi wa Tukuyu,Lutusyo Kabenjela (45) mkazi wa Kyela, Elizabeth Andwer(27)Dina Mwasongela (14) mwanafunzi wakidato cha tatu sekondari ya Lutengano Mbeya,Alex Mwaibambe (28) mwanafunziwa mwaka wa pili injinia katika chuo kikuu cha Dar es Salaaam ,Amon Luvanga(30) mkazi wa Mbeya,Yohana Mwasomola(28) Wengine ni Aggrey Mwangulu (56) mfanyakazi wa TRA Kibaha , Runna Mwampate (36) mkazi wa Kilawani Dar es Salaam , Iman Mwakifwage (32) mkazi wa Mbeya 
Mbali ya majeruhi hao kulazwa katika Hospital ya wilaya ya Mufindi baadhi ya majeruhi walikimbizwa katika Hospital ya wilaya ya Ilembula wilayani Njombe. Kaimu kamanda wa polisi mkoa wa Iringa Claus Mwasyeba alithibitisha kutokeakwa ajali hiyo na kuwa majeruhi Ramadhan Kipangule (28) mkazi wa TukuyuMbeya amefariki usiku wa leo wakati akipatiwa matibabu katika Hospital ya wilaya ya Mufindi. Alisema kuwa kati ya abiria waliokufa katika ajali hiyo watatu ni wanawake na abiria wawili ni wanaume na mmoja ametambuliwa kwa jina la ramadhan Kipangule (28) mkazi wa Uyole Mbeya . Hata hivyo alisema kuwa jeshi la polisi linaendelea kumsaka dereva wa basi hilo Yahaya Abdalla (35) mkazi wa Dar es Salaam na msaidizi wake Nasib Salum ambao baada ya ajali hiyo walikimbia.Mkuu wa wilaya ya Mufindi Evarista kalalu amewataka wananchi popote pale nchini kujitokeza kutambua miili ya marehemu hao akiwemo mwanamke huyo aliyeacha mtoto wa mwaka mmoja na nusu.

Sunday, January 29, 2012

WEMA AMZODOA DIAMOND MCHANA KWEUPEE..!!

Hatimaye mrembo na msanii Wema Sepetu, ameweka wazi kuwa hataki tena kutembea na masharobaro kwani mapenzi yao yanakuwa hayana malengo zaidi ya kuchezeana.

Akizungumza hivi karibuni msanii huyu alisema kuwa msanii anayemfananisha na sharobaro ni aliyekuwa mpenzi wake
Nassib Abdul ‘Diamond’, kwani endapo angekuwa hayuko hivyo basi anaamini mapenzi yao yangedumu kwa muda mrefu.

Alisema kwa sasa anahitaji kutoka na mwanaume aliyemzidi umri kwani anaamini watu hao wanakuwa na mapenzi ya dhati tena hawana wivu kama watoto wadogo ambao muda wote hupenda kuwa karibu na wapenzi wao badala ya kufanya kazi.


“Kila kitu kina muelekeo wake, mapenzi yangu mimi na Diamond yangeweza kudumu lakini kutokana na usharobaro alionao ndiyo uliosababisha yote yaliyotokea, na ndiyo maana nasema kwamba ni bora kutembea na mwanaume aliyekuzidi umri mnaweza kufika mbali,”
alisema.

Msanii huyu alisema hata hivyo ni bora afunge ndoa na mwanaume atakayempata ambaye anajua maana ya mapenzi kuliko kutembea na vijana wadogo ambao hawajui nini maana ya mapenzi na hawana muelekeo wa maisha.

BOSI WA TBS HATIANI KWA UDANGANYIFU

Muonekano mwingine व Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS), Charles Ekelege wakati wa kikao hicho
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS), Charles Ekelege (kushoto) akiwa hoi wakati Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma (PAC), Deo Filikunjombe (kulia), akimshutumu kwa utendaji wake mbovu, uliojaa utapeli ambao Kamati hiyo iliugundua katika ziara nje ya Nchi ya kukagua kampuni za ukaguzi wa magari yanayoingizwa nchini. Filikunjombe alikuwa anazungumza hayo katika kikao cha kamati za Bunge za Hesabu za Serikali (POAC) na PAC cha kujadili utendaji wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Dar es Salaam
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS), Charles Ekelege akizungumza na wanahabari baada ya sakata hilo, hata hivyo hakutaka kufafanua jambo lolote , hivyo kuamua kuondoka na kuwaambia kuwa wanahabari atakutana nao leo kuelezea kwa kina.
Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma (PAC), Deo Filikunjombe (kulia), akimshutumu Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS) Charles Ekelege (picha ya juu) kwa utendaji wake mbovu, uliojaa utapeli ambao Kamati hiyo iliugundua katika ziara nje ya Nchi ya kukagua kampuni za ukaguzi wa magari yanayoingizwa nchini. Filikunjombe alikuwa anazungumza hayo katika kikao cha kamati za Bunge za Hesabu za Serikali (POAC) na PAC cha kujadili utendaji wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Dar es Salaam
Mbunge Lugora akielezea jinsi alivyoaksilishwa na ubabaishaji wa Ekelega, na kuamua kumrushia konde ambalo lilidakwa na Filikunjombe wakiwa Ughaibuni baada kamati kupewa sumu feki ya kampuni ya nje inayokagua magari yanayoingizwa nchini
Mbunge wa Viti Maalum, Esther Bulaya (CCM), akielezea jinsi alivyotapeliwa na wakala wa ukaguzi wa magari
Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda, Biashara na Masoko,Joyce Mapunjo (katikati), akizungumza na Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma (PAC), Deo Filikunjombe (kushoto) na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (POAC), John Cheyo baada ya kamati hizo kumtajia uozo wa ukaguzi wa magari unaofanywa na Shirika la Viwango Tanzania (TBS) kwa kushirikiana na kampuni feki za nje ya Nchi,jana wakati wa vikao vya Kamati za Bunge, Dar EsSalaam.Picha na Mdau Richard Mwaikenda
--
KAMATI ya Bunge ya Mashirika ya Umma (POAC) imemlipua Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Viwango Nchini (TBS), Charles Ekelege baada ya kubaini kuwa shirika hilo lina ofisi hewa za ukaguzi wa magari nje ya nchi.

Imesema kutokana na hali hiyo fedha za ukaguzi zinazotolewa na wanunuzi wa magari, zinaishia mikononi wa wajanja huku ikisisitiza kuwa itaanika madudu mengine ya TBS katika kikao cha Bunge kinachoanza wiki ijayo na kwamba hali hiyo ndio chanzo cha kujazana kwa magari mabovu nchini. Akizungumza katika kikao cha Kamati ya Hesabu za Serikali, (PAC), Makamu Mwenyekiti POAC, Deo Filikunjombe alisema waligundua madudu hayo baada ya kamati yake kutembelea vituo vya ukaguzi wa magari nchini Singapore na mjini Hong Kong, China.

Wakati Filikunjombe akieleza hayo mbele ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda, Biashara na Masoko, Joyce Mapunjo, Ekelege alionekana kuishiwa nguvu na kupata mshangao. Mapema Mwenyekiti wa Kamati ya Hesabu za Serikali, John Cheyo alisema a walilazimika kuwaita wajumbe wa POAC katika kikao hicho kwa kuwa suala hilo ni nyeti. “Tulikwenda Hong Kong na Singapore na tumegundua kwamba TBS ni wababaishaji, huwezi kuamini anachokifanya Mkurugenzi (Ekelege) huko nje”,
“Ninasema haya bila woga wowote na hata nikiwekewa sumu, wajumbe wengine wa kamati yangu watasema,” alisema. Alisema walipotembelea Hong Kong, waligundua kuwa ukaguzi wa magari haufanyiki na kwamba fedha zinazotolewa na wanunuzi zinaliwa na wajanja.

Kwa mujibu wa kiongozi huyo wa kamati,Ekelege aliwapeleka katika ofisi hewa ambayo baadaye waligundua kuwa haikuwa ya ukaguzi wa magari. “Katibu (Mapunjo) ili ulinde heshima yako usimbebe Ekelege, tumekwenda Hong Kong na akatupeleka katika ofisi feki na tulipombana akasema kuwa aliomba kwa muda kuitumia ofisi hiyo,” alisema Filikunjombe. Alisema kampuni inayotumiwa na TBS kukagua magari nje ya nchi inapasaw ieleweke huku akifafanua kuwa wakati wakiwa Hong Kong, walinunua cheti feki cha TBS mtaani. “Huyu Ekelege si mkweli, ukaguzi wa magari haufanyiki sisi tumekwenda na kujionea wazi, ndio maana magari mengi yakifika hapa yanakuwa mabovu na gharama za usafirishaji na ukaguzi zinakuwa kubwa,” alisema Filikunjombe.

Kwa mujibu wa Filikunjombe baadhi ya watu waliowakuta katika kampuni hizo waliwaeleza kuwa Ekelege amekuwa akiwaeleza kwamba fedha za ukaguzi zinazopatikana wazitumie kununulia vifaa vya magari. Alisema walipokwenda Singapore pia hawakukuta kampuni ya kukagua magari na kwamba walipomuuliza Ekelege akashindwa kuwapeleka zilipo ofisi za ukaguzi wa magari. “Jamani mashirika yetu ya umma yananyonywa na wajanja wachache, fedha zinaliwa na wakati tupo huko tuliomba namba za simu na kupewa za uongo,” alisema Filikunjombe.

Alisema kama Mapunj) anambeba Ekelege, wao kama wabunge hawatakuwa tayari kuvumilia suala hilo huku akisisitiza kuwa wana mengi ya kuzungumza kuhusu mkurugenzi huyo. “Hayo ni machache sana kuna mengi ambayo kamati tumeyagundua katika ziara yetu na tutayaanika hadharani Dodoma,” alisema Filikunjombe.

Katika hali isiyokuwa ya kawaida Mbunge wa Mwibara (CCM), Kangi Lugora alisema walipokuwa nchini humo alitaka kupigana waziwazi na Ekelege baada ya kugundua jinsi walivyokuwa wakidanganywa kama watoto wadogo. Kwa upande wake Mbunge wa Viti Maalum (CCM), Ester Bulaya alisema a ripoti ya TBS inaonyesha kuwa ukaguzi wa magari ni Dola150 lakini ofisi hizo za ukaguzi zinataka zilipwe Dola300. “Mimi mwenyewe walitaka kunitapeli nilikuwa nataka kununua gari na wakanieleza niwatumie Dola300 wakati kawaida natakiwa kulipia Dola150, nilipowaeleza wakasema wana mtandao mkubwa na hata niende wapi siwezi kuwakamata,” alisema Bulaya.

Mapema Cheyo aliiponda ripoti ya TBS ya mwaka 2011 na kueleza kuwa ina upungufu mkubwa.
“Ripoti ina upungufu, kwanza haina takwimu zinazoonyesha magari mangapi yalikaguliwa na ukaguzi uliingiza fedha kiasi gani na zilizobaki ni kiasi gani” alisema Cheyo. Alisema licha ya taarifa ya CAG kueleza kuwa zoezi la ukaguzi wa magari halikufanyika ipasavyo, bado ukaguzi wa kucha bandia na nywele uliendelea kufanywa na kampuni hizo hewa.

“Hata vitu vilivyokaguliwa na kuonekana kuwa havifai haijulikani viko wapi, haijulikani kama vimetupwa ama laa, hakuna ushahidi vilikuwa kiasi gani” alisisitiza. Alisema kuwa kutokana na hali hiyo kamati yake haitaipitisha ripoti hiyo huku akimwagiza Mapunjo kuandaa upya ripoti hiyo na kuiwasilisha mbele ya kamati yake kabla ya Februari 2 na iwe imekaguliwa na CAG.

“Hakuna haja ya kuendelea kubishana tunaitaka wizara mpaka kufika Alhamisi ijayo (Februari 2) tupate takwimu zote na ziwe zimekaguliwa na CAG,” alisema Cheyo. Cheyo alimweleza Mapunjo kwamba kabla ya kumalizika kwa kikao cha Bunge mjini Dodoma watakutaka na Waziri wa Viwanda Biashara na Masoko na Kamati ya PAC na POAC ili kulijadili kwa kina suala hilo.

“Pia tutamweleza Spika wa Bunge ili kuona kama suala hili tunaweza kulifikisha bungeni ili wabunge watoe maoni yao,” alisema Cheyo. Ekelege anena Baada ya kikao hicho kumalizika Mwananchi lilimtafuta Ekelege ili ajibu tuhuma hizo ambapo alisema kuwa hawezi kuzungumza lolote huku akitaka atafutwe leo ofisini kwake.

Huku akionekana kuwa na kigugumizi Ekelege alisema,“Kwa leo siwezi kusema lolote kwa kuwa sina data (vielelezo), kesho (leo) njoo ofisini kwangu nitakueleza kila kitu, ila kwa sasa siwezi kusema lolote” alisema Ekelege Kauli ya Wizara Kwa upande wake Mapunjo alisema kuwa hawezi kueleza chochote kwa kuwa hajaipata ripoti ya CAG na kusisitiza kuwa atakapoipata ripoti atatoa ufafanuzi.

SERENGETI LAGER YAZINDUA NEMBO YENYE MUONEKANO MPYA WA DHAHABU, LAKINI BURUDANI ILEILE.

Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda Biashara na Masoko B. Joyce Mapunjo katikati akiwa katika picha ya pamoja na uongozi wa Kampuni ya bia ya Serengeti mara baada ya kuzindua rasmi bia ya Serengeti katika muonekano wa Dhahabu, uzinduzi uliofanyika jana jioni kwenye hoteli ya Golden Tulip jijini Dar es salaam na kuhudguriwa na wadau mbalimbali na wageni waalikwa.
Kutoka kulia ni Emilian Rwejuna meneja masoko (SBL) Mark Tyro Mkurugenzi wa Usambazaji, Ephraima Mafuru Mkurugenzi wa Masoko, Mgeni rasmi Katibu Mkuu Viwanda, Biashara na Masoko Joyce Mapunjo, Mkurugenzi mtendaji wa (SBL) Richard Wells na kushoto ni Zohra Moore Meneja wa Huduma IPP wakipozi kwa picha huku wakiwa wameshikilia chupa mpya ya Serengeti Lager iliyo katika muonekano wa Dhahabu
Chupa mpya ya Serengeti Lager yenye muonekano wa wa Dhahabu ikiibuka kutoka katika maji mara baada ya kuzinduliwa rasmi jana usiku.
Shamrashamra zikiendelea wakati nembo mpya ya bia ya Serengeti Lager ikizinduliwa jana.
Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda Biashara na Masoko B. Joyce Mapunjo akizungumza katika uzinduzi huo
Mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya bia ya Serengeti (SBL) Richard Wells akizungumza katika uzinduzi huo wakati alipomkaribisha mgeni rasmi.
Ephraima Mafuru Mkurugenzi wa Masoko kampuni ya bia ya Serengeti akizungumzia mafanikio mbalimbali yaliyopatikana katika taifa kupitia bia ya Serengeti Lager.
Mark Tyror Mkurugenzi wa Usambazaji kulia na Ephraima Mafuru Mkurugenzi wa Masoko kampuni ya bia ya Serengeti wakionyesha nembo mpya ya bia ya Serengeti Lager. Mrembo wa Serengeti Lager akipozi kwa picha na huku akionyesha Nembo mpya ya bia ya Serengeti Lager
Mkurugenzi wa Usambazaji Mark Tyro kushoto akipozi kwa picha na marafiki zake Kutoka kulia ni Mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya bia ya Serengeti (SBL) Richard Wells, Ephraima Mafuru Mkurugenzi wa Masoko kampuni ya bia ya Serengeti na Mwisho ni Meneja wa Mahusiano kampuni ya bia ya Serengeti Nandi Mwiyombela
Hapa ilibaki burudani tu.
Ephraima Mafuru Mkurugenzi wa Masoko kampuni ya bia ya Serengeti akiongea na mkurugenzi wa Extra Bongo Kamalade Ali Choki , kulia ni Meneja Masoko wa (SBL) Emilian Rwejuna.
Hapa mzuka ukapanda kidogo lakini yote ilikuwa burudani na uzinduzi wa muonekano wa Dhahabu katika burudani ileile ya Serengeti Lager.
Wageni waalikwa mbalimbali wakiwa katika uzinduzi huo.
Kikundi cha ngoma za asili kikitoa burudani katika uzinduzi huo.
Dada Ritah Mchaki meneja wa bia ya Tusker katikati akipozi na wadau kutoka kampuni ya bia ya Serengeti hebu wacheki pozi lao.
Mdau Bahati Singh kutoka kampuni ya bia ya Serengeti yeye ilikuwa mishemishe tu ili kuhakikisha mambo ya uzinduzi yanakwenda sawa.
Mikakati ikipangwa hapa Meneja wa kiinywaji cha Serengeti Lager Allan Chonjo katikati anaonekana akitoa maelezo kwa Mkurugenzi wa Kampuni ya bia ya Serengeti Richard Wells kushoto, huku akimsikiliza pamoja na Meneja Masoko wa kampuni hiyo Emilian Rwejuna kulia.
Rapa mahili wa Extra Bongo Maarufu kama Furgason akighani huku akmsikilizia mnenguaji mahiri wa bendi hiyo Aisha Madinda wakati alipokuwa akicheza.
Huo ndiyo muonekano wa dhahabu wenyewe kama unavyoonekana.
Wanenguaji wa bendi ya Extra Bongo wakifanya vitu vyao jukwaani.
Wadau kutoka R$R wakiwajibika kazini.
Wadau mbalimbali waliohudhuria katika uzinduzi huo