Pages

BRAND NEW MUSIC

metty magese

metty magese

Listen & Download

http://mdundo.com/a/32626

Wednesday, November 30, 2011

MISS UTALII PACHIMBIKA MAMLUKI WATIMULIWA

 Bodi ya wakurugenzi ya Miss Tourism Tanzania Organisation, yenye dhima ya kikomo ya kuandaa na kuendesha mashindano ya Miss Utalii Tanzania,imeendelea na safisha safisha ya viongozi na waandaaji wababaishaji na mamluki,baada ya kuwafutia kuwatimua waandaaji wa Miss Utalii Dodoma, imemfukuza aliyekuwa mpiga picha wa mashindano hayo katika kamati ya Taifa ya Miss Utalii Tanzania, Shaabani Mpalule,kwa tuhuma za umamluki na hujuma za mashindano hayo.
Kwa mujibu wa taarifa iliyo tolewa na Rais wa Mashindano hayo, Gideon Chipungahelo, sababu za kufukuzwa ikiwa ni mara ya tatu sasa,baada ya kuwa amefukuzwa mwaka 2008, na kurejeshwa mwaka 2011 mwanzoni na kufukuzwa mwezi July 2011, kisha akaomba msamaha na kurejeshwa mwezi septemba 2011 kwa majaribio.
Sababu za kufukuzwa ni pamoja na utovu wa nidhamu ulio tukuka,kokosa uaminifu, na umamluki wa kuhujumu shindano la Miss Utalii Tanzania. Baadhi ya utovu huo wa ni dhamu na maadili ni pamoja na tuhuma za kutaka kubaka washiriki, kuiba nyaraka za kampuni, kutumia jina la mashindano kujipatia huduma ,mali na hata fedha kwa maslahi binafsi. Kupigana na waandaaji na wanakamati kiasi cha kuharibu mali za watu na hoteli, kuiba mali za wajumbe na wanalamati wengine zikiwemo kamera na mashine za DVD.
Pia imethibitika kuwa ni mamluki ambaye anamaslahi na anatumiwa na waandaaji wa mashindano mengine hususani shindano la Miss Demokrasia ambalo,amekuwa akijaribu kuliandaa bila ya mafanikio, pamoja na hujuma nyingine amekuwa akisambaza mbalimbali za kutengeneza katika mitandao mbalimbali,wadhamini na hata baadhi ya vyombo vya habari ,kutishia warembo na hata kutoa vitisho mbalimbali kwa waandaaji wa ngazi za chini na wanakamati wengine. Aidha amekuwa kinara wa uvurugaji mashindano haya kwa kusambaza taarifa mbalimbali za kukashfu,kucha shindano na kuwachafua viiongozi ,washiriki,washindi na hata sanaa ya urembo na ustawi wa shindano hili na mengine nchini, Wakati wote akiwa mpigapicha wa mashindano haya amekuwa akitumia picha kuwatishia washiriki na kuwapa masharti ambayo ni kinyume cha maadili ili awepe picha. Wakati wote amekuwa na tabia za kutumia au kuweka maelezo tofauti na picha za matukio mbalimbali ya mashindano kwa lengo la kuchafua warembo na mashindano kwa ujuma.

  JERRY MURO YUKO HURU

Mwandishi wa habari aliepata misukosuko Jerry Muro akiongea na waandishi wa habari leo baada ya kuachiwa huru na mahakama ya hakimu mkazi Kisutu.
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Jijijini Dar es Salaam imemwachia huru na kuwafutia mashtaka aliyekuwa Mtangazaji wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) Jerry Muro pamoja na washtakiwa wenzake wawili ambao ni Edmund Kapama na Deogratius Mgasa waliokuwa wakikabiliwa na kesi ya kuomba rushwa ya tsh.10 milioni.


BREAKING NEWS; MCHEKESHAJI O'NEAL AFARIKI DUNIA

Breaking News - Patrice ONeal died Monday night
Comedian Patrice O'Neal died Tuesday morning ... as a result of a stroke he suffered back in October ... this according to his friends at the "Opie and Anthony" radio show.

O'Neal had been a staple in the comedy world for years -- and performed at the "Comedy Central Roast of Charlie Sheen" back in September.

O'Neal was a regular guest on the "Opie and Anthony" radio show -- and appeared on several TV shows such as "Chappelle Show," "The Office," and "Tough Crowd with Colin Quinn."

Opie just tweeted, "Yes it's true that our pal Patrice O'Neal has passed away. The funniest and best thinker I've ever known PERIOD."

MARIAM RAMADHANI MREMBO MWENYE NDOTO ZAKUWA MWANAMITINDO MKUBWA

 
 
 
 
 
 Mariam Ramadhani ni msichana mrembo anaependa tasnia ya urembo na Mitindo,tunachukua fulsa hii kumtambulisha kwenu wadau kama ilivyo ada ya UNIQUEENTERTZ kuwatambulisha modoz na warembo wapya katika duru husika kazi kwenu wadu.

WATANZANIA WAISHIO UK WAANDAA MAOMBI YA KUIOMBEA TANZANIA NA KUTIMIZA MIAKA 50 YA UHURU

Waandaaji wa maombi ya ya Miaka 50 ya Uhuru chini Uingereza ”Association of Tanzanian Christians in Europe(CITE)” Wakiwa na Mwl Christopher Mwakasege wakati wa Summer Confference 2009.
Mithali 14:34 Biblia inasema Haki ya Mungu huinua Taifa na huu ndio mstari wa kusimamia katika Maombi hayo yanayowajumuisha watanzania wote waishio nchini Uingereza Hususani katika jiji la London. Kwa Mujibu Wa Mchungaji Emmanuel Chatawe ambaye ni mmoja wa waratibu wa Maombi hayo maombi hayo yatahudhuriwa na Viongozi mbalimbali wa Serikali pamoja na viongozi wa dini kutoka madhehebu mbalimbali.

Tuesday, November 29, 2011

AKI AFUNGA MDOA NA MWANAMKE MREFU


Muigizaji marufu wa filamu barani Afrika AKI amevunja ukapela na kuchua jiko aka mke tayari kuanza safari ya ndoa katika maisha yake.
Aki amejizolea umaarufu mkubwa kutokana na umbo lake na umahiri wake katika tasnia ya filamu duniani.
Mambo yalikuwa hivi .


BREKING NEWS: JK ATIA SAINI MUSWADA WA SHERIA YA MABADILIKO YA KATIBA

http://sundayshomari.files.wordpress.com/2011/08/president-jakaya-kikwete_portrait.jpg

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete
leo, Jumanne, Novemba 29, 2011, ametia saini Muswada wa Sheria ya
Mabadiliko ya Katiba ya Mwaka 2011.
Hatua hiyo ya Mheshimiwa Rais kutia saini Muswada huo inakamilisha safari
ya kutungwa kwa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ya Mwaka 2011 baada ya Bunge
kuwa limepitisha Muswada huo uliowasilishwa na Serikali katika kikao
kilichopita cha Bunge.
Aidha, kutiwa saini kwa Muswada huo ili uwe Sheria ni hatua kubwa na muhimu
katika safari ya kutungwa kwa Katiba mpya ya Tanzania kama ilivyoahidiwa na Mheshimiwa Rais Kikwete katika salamu zake za Mwaka Mpya kwa wananchi Desemba 31, mwaka jana, 2010.
Pamoja na kutiwa saini hiyo bado Serikali itaendelea kusikiliza maoni na
mawazo ya wadau na wananchi mbalimbali kuhusu namna ya kuboresha sheria hiyo.
Hivyo, Mheshimiwa Rais Kikwete anatoa wito kwa mwananchi yoyote mwenye
maoni ama mawazo ya namna ya kuboresha Sheria hiyo, ajisikie yuko huru
kutoa maoni yake na Serikali itasilikiza na kuchukua hatua zipasazo.

Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.
29 Novemba, 2011.



KILIMANJARO STARS YAITANDIKA DJIBOUTI MABAO 3:0

HATIMAE KILIMANJARO STARS IMEFANIKIWA KUPATA USHINDI WA KWANZA KWENYE MASHINDANO YA CECAFA TUSKER CHALLENGE CUP 2011 BAADA YA KUIFUNGA DJIBOUTI MABAO 3-0.
MABAO HAYO YAMEFUNGWA NA THOMAS ULIMWENGU,MWINYI KAZIMOTO NA YUSUF RASHID.
WAKATI HUO HUO RWANDA IMEIFUNGA ZIMBABWE MABAO 2-0 KWENYE MCHEZO ULIANZA MAPEMA.


SOKO LA KISIMANI MJI MDOGO WA TUNDUMA LILIVYOTEKETEA KWA MOTO.


Soko la Kisimani lililopo mji mdogo wa Tunduma, wilaya ya mpya ya Momba mkoani Mbeya limeteketea kwa moto hapo jana kuanzia majira ya Saa 10 jioni na kusababisha hasara kubwa ambapo vibanda vya biashara na maduka yameteketea kwa moto huo. Chanzo hakijaweza kubainishwa lakini inadaiwa kuwa Umeme uliporudi baada ya kukatika ndipo moto ulipoanza katikati ya Soko hilo
Vibanda vilivyokuwa vimejengwa kwa mbao vimeteketea na kubakia masalia ya mabati yaliyotumika kuezekea vibanda hivyo katika Soko la Kisimani lililopo mji mdogo wa Tunduma, wilaya ya mpya ya Momba mkoani Mbeya, jana kuanzia majira ya Saa 10 jioni na kusababisha hasara kubwa ambapo vibanda vya biashara na maduka yameteketeakwa moto huo.


Magari ya kampuni ya Ujenzi wa barabara ya Tunduma mpaka Sumbawanga yalifika kutoa msaada wa kudibiti moto katika Soko la Kisimani lililopo mji mdogo wa Tunduma, wilaya ya mpya ya Momba mkoani Mbeya lililoteketea kwa moto hapo jana kuanzia majira ya Saa 10 jioni na kusababisha hasara kubwa ambapo vibanda vya biashara na maduka yaliteketea
Mzee huyu alishikwa na bumbuwazi la kutoamini duka lake likiteketea kwa moto ambapo hivi karibuni aliingiza mzingo wa bidhaa kutoka jijini Dar es salaam uliogharimu shilingi milioni Ishirini

MARIAM RAMADHANI MWANAMITINDO MPYA ALIEPANIA KUWIKA

   Ramadhani ni mrembo mwenye ndoto zakuwa mwanamitindo mkubwa nchini Tanzania, ana umri wa miaka 19 tu,elimu yake ni kidato cha nne,hobi zake ni Mitindo na kuangalia muziki.
   Kitu apendacho ni Amani na kitu asichopenda ni ile tabia ya mtu kumfuatilia maisha yake kwa ujumla,rangi aipendayo ni bluu bahari na nyeupe na yuko ndani ya uhusiano wa kimapenzi na Boyfriend wake ambe kampata hivi karibu baada ya kuacha na na wale wa awali ambapo aliiambia  UNIQUEENTERTZ kuwa alishawahi kuwa na wavulana watatu kabla hajampata huyu wa sasa.
   Mariam ni mnyamwezi kwa kabila anaishi kulasini na matarajio yake ya baadae ni kuwa mjasiliamali wa kitaifa akiwa na lengo la kuishi maisha bora kwa nguvu zake mwenyewe.


 USHER NA MTALAKA WAKE HAPATOSHI
  Usher and Tameka Raymond
Usher
's ex-wife wants to take away his kids ... claiming the singer has repeatedly blown off his legal obligations as a co-parent ... and even worse -- he CLOSED her Saks 5th Avenue credit card ... this according to court docs obtained by TMZ.

Tameka Raymond -- who had 2 kids with Usher during their brief 2 year marriage -- filed court papers in Georgia ... asking a judge to strip Usher of joint physical custody of their children ASAP.

According to the docs, Tameka claims Usher has repeatedly FAILED to obtain her permission to travel outside the state with the kids ... which he's legally obligated to do.  


Monday, November 28, 2011

TWANGA PEPETA YAKONGA MIOYO MIAKA 50 YA UHURU LONDON


 African Stars Entertainment Tanzania (Aset) ambao wanajulikana kwa jina la  “Twanga Pepeta” walikuwa  kivutio cha sherehe za miaka 50 ya Uhuru London juzi Jumamosi. 
Kikosi hiki cha watumbuizaji maarufu wa Kibongo kilikaribishwa na  Urban Pulse, Jestina George wakishirikiana na Ubalozi wa Tanzania mjini hapa.
Watanzania wa kila rika, nasaba na taaluma walifurika toka miji ya Leeds, Bristol, Birmingham, Northampton, Milton Keynes na vitongoji mbalimbali kufurahia vigongo vya bendi hili lenye makao makuu Mango, Kinondoni Dar es Salaam. 
Ukumbi wa Club 2000 Banqueting Suite ulioko nyuma ya uwanja maarufu wa Wembley ulishuhudia tafrija hiyo wakati viongozi rasmi wa serikali walipofungua tafrija wakicheza nyimbo maarufu za Kitanzania kama ule wa mwanamuziki Salum Abdallah (“Wanawake wa Tanzania” na “Tujenge Nchi Yetu”) marehemu alizoimba mara baada ya Uhuru mwaka 1961.



JASIRI HAACHI ASILI

Makamu wa Rais Mh. Bilal akiwa na Waziri Mkuu akimpa maelekezo kuhusu mila za makabila ya Mkoa wa Rukwa na vitu wanavyotumia vya makabila ya huko.

 

MVUA YAKATA MAWASILIANO YA BARABARA KATI YA ARUSHA NA KARATU

Mawe yakiwa yamezolewa na maji hadi kuingia sehemu ya barabarani.

Hali ndiyo hii mdau.


Wananchi pamoja na watalii wanaotumia barabara inayo unganisha arusha na karatu leo wamekwama baada ya mto kirurumo uliopo mto wa mbu kukata barabara na kujaza mawe njiani vilele kwa mujibu wa wananchi waeneo hilo inasemekana mtu mmoja amepoteza maisha mto huo umefurika baada ya mvua kubwa iliyo nyesha usiku wa kuamkia leo.
Mwili wa marehemu Samweli Julius ambaye alikuwa ni msaidizi wa mitambo ya kutengeza barabara, ukiwa umenasa juu ya mti. 

STAR WA TLC (T-BOZ) AFILISIKA

  Tboz is bankrupt
T-Boz ain't too proud to beg -- just like TLC sang back in the 90s -- because she's filed for bankruptcy.

According to docs filed last month in U.S. Bankruptcy Court, T-Boz (real name Tionne Watkins) found herself owing creditors $768,642.99 -- mostly from mortgages on her $1.2 million house.

The docs don't paint a picture of exorbitant spending -- she takes in $11,700/month in income, with monthly expenses totaling $8,821.

TLC had ten top ten singles, four number one singles, four multi-platinum albums, and four Grammy Awards ... but according to the docs, T-Boz only pulls in $1,200/month in royalties.

T-Boz might have dodged the bankruptcy bullet if she'd been able to collect the child support she claims she's owed -- which according to the docs is $250,000.

 

EXCLUSIVE: KOCHA MPYA WA SIMBA MILOVAN CIRKOVIC ALIPOWASILI BONGO JANA

Baada ya kuwasili nchini, kocha Mserbia Milovan Cirkovic akilakiwa na katibu mkuu wa klabu ya Simba Evodius Mtawala kulia, na mwenyekiti wa kamati ya Ufundi ya klabu hiyo Ibrahim Masoud "Maestro" na wa mwisho kushoto ni Jerry Yambi mjumbe wa kamati ya mashindano ya klabu hiyo.
Kocha Mserbia Milovan Cirkovic aliyewasili nchini jana usiku kwa mazungumzo ya kuinoa timu yake ya zamani Simba sports club mara baada ya kuwasili uwanja wa ndege wa Dar es salaam, ambapo alipokewa na mwenyekiti wa kamati ya ufundi ya klabu hiyo Ibrahim Masoud "Maestro" kulia, wengine ni daktari msaidizi Shindika na Kit Manager Kessy.

Sunday, November 27, 2011

WABUNIFU WA TANZANIA WAFANYA KWELI MARYLAND USA




Mambo ya mitindo mdau nje ya nchi.






           Kwa staili hii tutafika mbali katika kiwanda cha mitindo.




MISS TOURISM TANZANIA KWENDA UTURUKI

Mshindi wa tano wa fainali za taifa za Miss Utalii Tanzania2010/2011 Sophia Dio na mshindi wa taji la vipaji la Miss Utalii Tanzania 2010/2011 Dessy Mushumbuzi,wanatarajia kuondoka nchini 19-12-2011 ,kwenda kuwakilisha Tanzania katika mashindano ya Dunia ya Miss Globe International 2011.

Jumla ya nchi 120 Duniani zinashiriki katika shindano hilo,litakalofanyika 30-12-2011 katika jiji la Istanbul na kuonyeshwa Live kupitia TV mbalimbali Duniani. Shindano hilo kama lilivyo shindano la Miss Utalii Tanzania,linalenga kutangaza na Utalii,Utamaduni wa mataifa mabalimbali Duniani,pia kuunganisha na kubadilishana tamaduni miongoni mwa mataifa na washiriki.

Hii itakuwa ni fulsa nyingine kwa Tanzania kuweza kutangaza utalii na utamaduni wetu kimataifa, na hata mianya ya uwekezaji iliyopo Tanzania kupitia warembo hawa wa Miss Utalii Tanzania, ambao historia inaonyesha kuwa mara zote wanaposhiriki mashindano ya Dunia na kimataifa hutwaa mataji mbalimbali. hadi sasa Miss Utalii Tanzania tunashikilia zaidi ya mataji 5 ya Dunia,yakiwemo Miss Tourism World 2005- Africa, Miss Tourism World 2006 -SADC, Miss Tourism World 2007 - Africa, Model Of The World 2008 - Personality , Miss Africa 2006 - !ST Runner Up n.k

Tunaendelea na maandalizi kuhakikisha tunadumisha na hata kuvuka rekodi ya kwa kuahalilisha kuwa warembo hao wanarudi na mataji na sio wasindikizaji kama walivyo wengine. Tunaomba makampuni na watu mabalimbali wajitokeze kudhamini na kuchangia safari na ushiriki wa warembo hao katika mashindano hayo ya Dunia